NAFASI YA KATIBU MKUU - TUCTA KUWA WAZI

NAFASI YA NAIBU KATIBU MKUU – TUCTA KUWA WAZI

Tarehe 25 Januari 2023, Mh.Dkt. Samia Suluhu Hassan,Rais wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania alifanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya Nchini, ambapo

aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu TUCTA, Ndugu Cornel L. Magembe aliteuliwa na

kuwa Mkuu wa Wilaya ya Geita. Hivyo kufanya nafasi ya Naibu Katibu Mkuu

kuwa wazi. Aidha, Kikao cha Kamati ya Utendaji kilifanya Uchaguzi mdogo

ambapo Ndugu Saidi S. Wamba alikaimishwa nafasi ya Naibu Katibu Mkuu

hadi hapo Baraza Kuu litakapofanya uchaguzi kwa nafasi hiyo kwa mujibu wa

Katiba ya TUCTA.